Jaji Salome Kaganda: Siitambui barua iliyotumwa kwa Mbowe, Lissu wakitakiwa kujieleza mbele ya tume.

Jaji Salome Kaganda: Siitambui barua iliyotumwa kwa Mbowe, Lissu wakitakiwa kujieleza mbele ya tume::

Hatimaye kamishna mkuu wa tume ya maadili kwa watumishi wa umma Jaji Salome Kaganda ameikana barua iliyosomwa jana na katibu mkuu wa Chadema Dr Vincent Mashinji ambayo inadaiwa kutoka katika tume hiyo na iliyosainiwa na kamishna huyo kuwataka Mbowe na Tundu Lissu kujieleza ndani ya siku 21 kuwa ni kwanini wasichukuliwe hatua kutokana na kukiuka maadili ya utumishi wa umma.

Jana nilifananisha neno "utangamano" lililotumika ndani ya barua ile na neno linalotumiwa sana na kiongozi mmoja mkuu wa nchi huku nikielezea dukuduku langu kuwa huenda barua ile iliandikwa na yeye na siyo Jaji Salome Kaganda kama inavyodaiwa.

Chanzo ni Tanzania Daima la leo jumatano tarehe 10 August 2016

By G Sam
Source JF

No comments:

Powered by Blogger.