Breaking News: TCU Yakifuta Chuo Kikuu cha St. Joseph Kampasi ya Arusha.......Wanafunzi Watahamishiwa Vyuo Vingine


1.Tunapenda kuuarifu umma kwamba, Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu
Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha ni mojawapo ya vyuo vikuu vilivyosajiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ambacho kilianza kudahili wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka wa masomo 2013/2014.


2.Kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania, Tume ina mamlaka ya kusimamia na kudhibiti ubora na usimamizi wa uendeshaji wa Vyuo Vikuu hapa nchini.


3.Kwa muda mrefu na kwa wakati tofauti kumekuwapo na matukio ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha na wanafunzi. 

Kwa kipindi hiki chote Tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo kwa uongozi wa chuo kurekebisha kasoro zinazosababisha migogoro chuoni hapo.

Kwa sehemu kubwa migogoro hiyo imekuwa ikitokana na matatizo ya ubora, uongozi, ukiukwaji wa sheria na taratibu za uendeshaji wa chuo kikuu kama zilivyobainishwa na Sheria ya Vyuo Vikuu. 

Hata hivyo jitihada za Tume ya Vyuo Vikuu kukitaka Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa katika Kampasi hii inakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Tume hazikupewa uzito stahiki na uongozi wa chuo.


4.Hivi sasa Kampasi ya Arusha ina jumla ya wanafunzi 1557 wanaosoma programu za masomo ya ualimu wa sayansi zifuatazo:

 
1.Tunapenda kuuarifu umma kwamba, Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha ni mojawapo ya vyuo vikuu vilivyosajiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ambacho kilianza kudahili wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka wa masomo 2013/2014.


2.Kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania, Tume ina mamlaka ya kusimamia na kudhibiti ubora na usimamizi wa uendeshaji wa Vyuo Vikuu hapa nchini.


3.Kwa muda mrefu na kwa wakati tofauti kumekuwapo na matukio ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha na wanafunzi. 

Kwa kipindi hiki chote Tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo kwa uongozi wa chuo kurekebisha kasoro zinazosababisha migogoro chuoni hapo.

Kwa sehemu kubwa migogoro hiyo imekuwa ikitokana na matatizo ya ubora, uongozi, ukiukwaji wa sheria na taratibu za uendeshaji wa chuo kikuu kama zilivyobainishwa na Sheria ya Vyuo Vikuu. 

Hata hivyo jitihada za Tume ya Vyuo Vikuu kukitaka Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa katika Kampasi hii inakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Tume hazikupewa uzito stahiki na uongozi wa chuo.


4.Hivi sasa Kampasi ya Arusha ina jumla ya wanafunzi 1557 wanaosoma programu za masomo ya ualimu wa sayansi zifuatazo:

 
PROF. YUNUS D. MGAYA
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania 
26 Februari 2016

No comments:

Powered by Blogger.