Alichokizungumza Mchezaji Samatta Baada ya Kufunga Goli Mbili Europa League


Samatta akiwa na timu yake ya KRC Genk ambao walikuwa ugenini usiku wa March 9 kucheza mchezo wao wa kwanza wa Europa League hatua ya 16 bora dhidi ya KAA Gent, Samatta anarudi katika historia baada ya kufanikiwa kuifungia goli mbili KRC Genk dhidi ya KAA Gent katika ushindi wa 5-2.

Baada ya hapo Samatta ambaye kacheza mechi yake ya 9 ya Europa League ndio kafunga goli, alifanya mahojiano  na Sport Extra ya Clouds FM na kueleza anavyojisikia kufanikiwa kufunga katika michuano ya UEFA Europa League hatua ya 16 bora.

“Nakosa hata cha kusema kwa jinsi ninavyojisikia kwa sababu nilikuwa natafuta sana hilo goli la Europa kuliko kitu chochote, nilikuwa nahangahika na kipindi ambacho natafuta hayo magoli yalikuwa hayaji, kwa hiyo ile game ya jana ilikuwa nimeshatafuta sana magoli kwa hiyo nikaona bora ni relax ikitokea nafasi sawa”

No comments:

Powered by Blogger.