Wakala_wa_Shetani -6..
KWA TAARIFA
ZAIDI NICHEKI HAPA 0785848566
ILIPOISHIA;
Wazo alilokuwa nalo lilikuwa ni kukiulia mbali kile kitoto na kumweleza mkewe kuwa kilindondokea kwenye maji.
Lakini aliamini mkewe hawezi kumwamini hasa baada ya kutaka kumuua mara ya kwanza.
Alijua chochote kibaya hata kama cha bahati mbaya kitaonekana ni cha makusudi.
SASA ENDELEA...
Wazo alilokuwa nalo lilikuwa ni kukiulia mbali kile kitoto na kumweleza mkewe kuwa kilindondokea kwenye maji.
Lakini aliamini mkewe hawezi kumwamini hasa baada ya kutaka kumuua mara ya kwanza.
Alijua chochote kibaya hata kama cha bahati mbaya kitaonekana ni cha makusudi.
SASA ENDELEA...
Hali ya kusimama kwa muda mrefu
huku akimbeba mtoto bila sehemu ya kukaa ilimte ,sa sana. Kutokana na kujaa maji na matope kila sehemu,
hakukuwa na sehemu ya kumweka mtoto ili apumzike. Aliona mateso yale yalikuwa
ni ya kujitakia, aliamini hakukuw na haja ya kuteseka kama wangemuulia mbali
yule mtoto.
Baridi lilikuwa kali mpaka
likaanza kumwingia tumboni na kuzidi kumweka kwenye wakati mgumu. Kuna wakati
alichoka sana na kuamua kutafuta sehemu yenye mwinuko kidogo na kukaa ndani ya
maji.
Kila mateso yalivyozidi kumpata
alizidi kumchukia yule mtoto na kufikia kuwaza kwenda kwa siri kwa wana kijiji
kuwaeleza habari za mkewe kujifungua mtoto Albino ili achukuliwe na kuuawa.
Aliamini ile ndiyo njia itakayowafanya waishi maisha ya amani. Pamoja na kuyawaza yote, bado aliamini mkewe lazima atamfikiria vibaya. Alijuta kutoa wazo la kumuua yule mtoto, aliamini kama angekaa kimya mkewe asingejua mpango wake, hivyo, ingemrahisishia kutimiza dhamira yake bila mkewe kujua.
Aliamini ile ndiyo njia itakayowafanya waishi maisha ya amani. Pamoja na kuyawaza yote, bado aliamini mkewe lazima atamfikiria vibaya. Alijuta kutoa wazo la kumuua yule mtoto, aliamini kama angekaa kimya mkewe asingejua mpango wake, hivyo, ingemrahisishia kutimiza dhamira yake bila mkewe kujua.
Kilichomchanganya zaidi akiwa
katikati ya dimbwi la mawazo, mtoto alianza kulia tena kwa sauti ya juu.
Wasiwasi wake mkubwa kama atatokea mpita njia lazima angemsikia na kusogea.
Alijitahidi kumbembeleza lakini mtoto aliendelea kulia.
Alijiuliza mkewe kachelewa wapi au njia imefunga kutokana na maji kuwa mengi, alipata wazo la kumfuata mkewe akiwa na mtoto wao na mengine yangejulikana hukohuko.
***
Alijiuliza mkewe kachelewa wapi au njia imefunga kutokana na maji kuwa mengi, alipata wazo la kumfuata mkewe akiwa na mtoto wao na mengine yangejulikana hukohuko.
***
Wakati mama Sabina akimtafakari
Ng’wana Bupilipili na mumewe, juu ya mabadiliko alioyaona juu yake.
Pia, mumewe na mawazo mabaya kwa mtoto wao. Ngw’ana Bupilipili alikuwa njiani kurudi shamba alipomuacha mumewe na mtoto. Ilibidi apite njia ileile ya kuingia ndani ya mito na vidimbwi vya maji ambavyo vilikuwa havikwepeki.
Pia, mumewe na mawazo mabaya kwa mtoto wao. Ngw’ana Bupilipili alikuwa njiani kurudi shamba alipomuacha mumewe na mtoto. Ilibidi apite njia ileile ya kuingia ndani ya mito na vidimbwi vya maji ambavyo vilikuwa havikwepeki.
Alishangaa kukutana na mumewe
njiani, ile ilimshtua na kumuuliza.
“Vipi mbona huku unakwenda wapi?”
“Nilikuwa nanyoosha miguu kidogo kukaa sehemu moja nilichoka,” Mathayo alidanganya.
“Mume wangu unakuja huku watu wakimuona utanibebea mbeleko gani?” Ngw’ana Bupilipili alimlalamikia mumewe.
“Mke wangu nisingefika mbali.”
“Mmh! Sawa, vipi ameanza kulia muda mrefu?”
“Si mrefu sana lakini nilichanganyikiwa nashukuru umerudi haraka, sijui ungechelewa ningemfanyaje?”
“Inawezeka amekojoa,” Ngw’ana Bupilipili alisema huku akimchukua mwanaye, mwili wote ukiwa umetoka maji na kuhisi baridi kali.
“Vipi mbona huku unakwenda wapi?”
“Nilikuwa nanyoosha miguu kidogo kukaa sehemu moja nilichoka,” Mathayo alidanganya.
“Mume wangu unakuja huku watu wakimuona utanibebea mbeleko gani?” Ngw’ana Bupilipili alimlalamikia mumewe.
“Mke wangu nisingefika mbali.”
“Mmh! Sawa, vipi ameanza kulia muda mrefu?”
“Si mrefu sana lakini nilichanganyikiwa nashukuru umerudi haraka, sijui ungechelewa ningemfanyaje?”
“Inawezeka amekojoa,” Ngw’ana Bupilipili alisema huku akimchukua mwanaye, mwili wote ukiwa umetoka maji na kuhisi baridi kali.
Alimpakata mwanaye na kuanza
kumnyonyesha, hapakuwa na sehemu ya kukaa kutokana na kila kona kujaa maji.
Yalikuwa nki mateso mazito sana katika maisha yao.
Walikubaliana kurudi nyumbani
kiza kikiingia ili kumpeleka mtoto kwenye joto kwa kuogopa mtoto kupatwa na
ugonjwa wa Nimonia.
Waliendelea kuvumilia kukaa kule shamba pamoja na baridi kali pia wingu zito likitanda tena kuonesha mvua ingeteremka tena wakati wowote.
Waliendelea kuvumilia kukaa kule shamba pamoja na baridi kali pia wingu zito likitanda tena kuonesha mvua ingeteremka tena wakati wowote.
Ng’wana Bupilipili alimuomba
Mungu kwa kila lugha aliyoifahamu ili mvua isishuke kwa kuamini lazima mtoto
wao watampoteza kwa baridi au kufa maji. Alijua kama mvua itanyesha muda ule
lazima hata maisha yao yatakuwa mashakani kwa kushindwa kuona sehemu
watakayojificha kutokana na kiza kilichoanza kutanda tena.
Baridi lilizidi kuwa kali huku
wakimkumbatia mtoto wao kwa kumweka kati ili apate joto la wazazi wake,
kutokana na ubaridi kuwa mkali na sehemu ya kukaa haikuwepo, ilikuwa ni adhabu
kubwa sana kwao kusimama kwa muda mrefu bila kukaa huku wakipokezana kumbeba mtoto.
***
***
Usiku uliingia wakiuona huku
wakiwa hoi kama wapo kwenye adhabu. Mathayo bado aliamini ule ni mkosi kutokana
na kukiuka masharti ya kumficha yule mtoto Albino. Lakini aliogopa kumweleza
mkewe kwa kuamini hatakubaliana na chochote atakachomweleza.
Kiza kilipoingia waliongozana na
mtoto wao huku wakitetemeka kurudi kijijini kwa kuingia kwenye vidimbwi vya
maji kuna kipindi walipita kwenye maji yaliyowafikia vifuani.
Ilikuwa adhabu kubwa kama
ingekuwa amri ya Mathayo angemtupa mtoto ili afie mbali na yeye kurudi kijijini
bila hata mshipa wa fahamu kumgonga kama amepoteza damu yake. Aliamini tabu
yote ile isingewafika kama wangekubali kumtoa mtoto wao na kuuawa.
Wasiwasi wake kama kijiji kitajua
kuwa mkewe amejifungua mtoto albino, basi wangetengwa pia kutozwa faini ya
ng’ombe na kuchukuliwa sehemu ya shamba. Alimuona mkewe kama anataka kumitia
kwenye umaskini kwa kunyang’anywa mali zake kwa ajili ya mtoto ambaye hata
wakimficha lazima angeonekana tu, kwani lazima amgelia na sauti ingesikika kwa
watu.
Walirudi nyumbani kwa taadhari
kubwa huku mkono wa Ng’wana Bupilipili ukiwa hauchezi mbali na mdomo wa mtoto
wake ili akitaka kulia amzibe mdomo asitoe sauti.
Walifanikiwa kuingia ndani kwao bila mtu yeyote kuwaona. Baada ya kuingia ndani waliwasha moto ambao waliuota na miili yao kupata joto kisha waliandaa chakula cha usiku.
Walifanikiwa kuingia ndani kwao bila mtu yeyote kuwaona. Baada ya kuingia ndani waliwasha moto ambao waliuota na miili yao kupata joto kisha waliandaa chakula cha usiku.
Muda ulikuwa umekwenda sana,
ilikuwa inakimbilia saa tatu usiku. Lakini ilionekana ni kama saa sita za usiku
kutokana na kiza na wingu zito la mvua.
Baada ya kula walichemsha maji ya
moto na kwenda kuoga kutokana na kushinda na kupita kwenye maji machafu.
Kwa vile mtoto alikuwa amelala baada ya kunyonya na kushiba. Walikwenda kuoga kwa pamoja, wakiwa wanaoga mtoto alianza kulia na kutoa sauti ambayo kutokana na utulivu wa usiku ilifika mbali.
Kwa vile mtoto alikuwa amelala baada ya kunyonya na kushiba. Walikwenda kuoga kwa pamoja, wakiwa wanaoga mtoto alianza kulia na kutoa sauti ambayo kutokana na utulivu wa usiku ilifika mbali.
Ngw’ana Bupilipili aliposikia
sauti ya mtoto aliacha kuoga hata bila kukumbuka nguo alitoka mbio kuwahi
kumnyamazisha. Kwa vile ilikuwa kiza hakuna ambaye alimuona ametoka bila nguo.
Alipofika alimbeba mtoto wake na
kuanza kumnyonyesha huku akimbembeleza, ilionekana alikuwa amejikojolea na
kutokana na hali ya baridi ilimfanya alie.
Baada ya kunyonya na kumbadili nguo alinyamaza na kupitiwa tena na usingizi.
Baada ya kumlaza alirudi bafuni na kumalizia kuoga, wakati huo mumewe alikuwa ameishamaliza kuoga na kukaa na mtoto.
****
Baada ya kunyonya na kumbadili nguo alinyamaza na kupitiwa tena na usingizi.
Baada ya kumlaza alirudi bafuni na kumalizia kuoga, wakati huo mumewe alikuwa ameishamaliza kuoga na kukaa na mtoto.
****
Mama Sabina usiku ule alikuwa
akiangalia mifugo kabla ya kulala, alisikia sauti ya mtoto akilia, lakini
hakuwa na uhakika inatoka wapi.
Sauti ilimjulisha ni mtoto mchanga na eneo lile hakukuwepo na mtoto mchanga. Baada ya kuhakikisha mifugo ipo tayari alirudi ndani ambako mumewe alikuwa amekwishatangulia kitandani.
Sauti ilimjulisha ni mtoto mchanga na eneo lile hakukuwepo na mtoto mchanga. Baada ya kuhakikisha mifugo ipo tayari alirudi ndani ambako mumewe alikuwa amekwishatangulia kitandani.
“Mume wangu nimesikia sauti ya
mtoto mchanga akilia,” alisema huku akirudisha mlango kabla ya kupanda
kitandani.
“Mtoto mchanga?” mumewe alishtuka huku akigeuka.
”Eeh.”
“Sasa tatizo nini?”
”Unajua hapa kitongojini kwetu aliyekuwa na ujauzito wa kujifungua ni mke wa Mathayo Ngw’ana Bupilpili.”
“Mtoto mchanga?” mumewe alishtuka huku akigeuka.
”Eeh.”
“Sasa tatizo nini?”
”Unajua hapa kitongojini kwetu aliyekuwa na ujauzito wa kujifungua ni mke wa Mathayo Ngw’ana Bupilpili.”
Itaendelea
No comments: