Uganda yafunga mitandao ya kijamii
Uganda imefunga mitandao ya kijamii imefungwa
kote nchini humo katika siku ya uchaguzi wa urais.
Rais Yoweri Museveni
amejitetea akisema nia ya serikali yake ni kuzuia waganda kueneza uongo kuhusu
uchaguzi mkuu unaoendelea .
Mitandao ya Facebook,
Twitter, Whatsapp na huduma za kutuma na kupokea pesa zimefungwa.
Licha ya hatua hiyo
iliyokosolewa na waganda wengi,kibwagizo cha #UgandaDecidesis kingali kinapata
umaarufu mkubwa haswa kwenye mtandao wa Twitter.
Vilevile penye nia
pana njia,waganda wengi akiwemo kiongozi wa upinzani na muaniaji kiti cha urais
Amama Mbabazi wamepata njia mbadala ya kuwasiliana wakitumia anuani ya mtandao
binafsi ya VPN - ( Virtual Private Network)
VPN ni NINI ?
VPN ni njia ambayo
kifaa cha kielektroniki kinaweza kutumia anuani binafsi ya mtandao unaotumika
katika mataifa jirani kama vile Kenya Sudan kusini na hata Marekani.
Mkuu wa idara
inayothibiti sekta ya mawasiliano nchini Uganda bwana Godfrey Mutabazi,
ameiambia BBC kuwa hatua ya kufunga mitandao ya kijamii imechukuliwa kufuatia
ombi la baraza linalosimamia uchaguzi nchini Uganda.
Mutabazi amesema kuwa
mitandao hiyo imefungwa ilikuzuia watu kuitumia kutuma hongo ili kuwashawishi
wapiga kura.
Kampuni inayoongoza
kwa wingi wa watumiaji ni MTN, ambayo inazaidi ya wateja milioni 10.
MTN imethibitisha kuwa
imeamrishwa ifunge huduma hizo za mitandao ya kijamii.
Waganda wengi walikuwa
wamekwenda kwenye mitandao ya kijamii kuelezea hasira zao baada ya vituo vya
kupigia kura kuchelewesha kuanza kwa shughuli ya uchaguzi kwa zaidi ya hata saa
5.
Tume ya uchaguzi
imekiri kuwa ilikabiliwa na changamoto nyingi katika usafirishaji wa makaratasi
ya uchaguzi.
Museveni anakabiliwa na wapinzani 7 katika uchaguzi huu.
Hata hivyo mpinzani
wake mkuu kanali mstaafu Kizza Besigye anadai uchaguzi huu hauendeshwi katika
njia ya ukweli na uhuru.
Vilevile bwana
Museveni anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa aliyekuwa mwandani wake wa
karibu kwa miaka mingi bwana Amama Mbabazi.
Mbabazi aliwahi
kuhudumu katika nyadhfa nyingi tu ikiwemo waziri mkuu kabla ya kufutwa kazi
alipodhaniwa kupinga sera za Museveni.
No comments: