Bao la mapema laipeleka Simba SC kileleni

Klabu ya Simba SC leo imefanikiwa kupanda kileleni baada ya kuitungua klabu ya Mbeya City goli 1-0 kunako uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Goli la Simba limefungwa na mshambuliaji wake, Shiza Kichuya mapema kunako dakika ya 8 kipindi cha kwanza. Kwa sasa klabu ya Simba inaongoza Ligi kuu Vodacom Tanzania Bara kwa pointi 19 ikifuatiwa na Azam FC yenye alama 19 wakitofautiana kwenye magoli ya kufunga na kufungwa huku Klabu ya Yanga ikishuka hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara kwa alama 17.

No comments:

Powered by Blogger.