Tetesi profesa lipumba adaiwa kujiunga ACT wazalendo

Kwa muda wa takribani saa kadhaa sasa kumekuwa na taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuwa aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na mwenyekiti mwenza wa UKAWA, Prof. Ibrahim Lipumba amejiunga na chama cha ACT- Wazalendo.

Taarifa hizo zimeenda mbali na kueleza kuwa, muda huu kuna kikao kinafanyika juu ya uamuzi wa ACT kumchukua Prof. Lipumba na kuwa mwenyekiti wa sasa wa ACT, Mama Anna Mghwira ajiandae kupisha nafasi hiyo.

Chama cha ACT- Wazalendo hakijatoa taarifa yoyote kuhusu tetesi hizi na wala Prof. Lipumba hajazungumza juu ya hili.

No comments:

Powered by Blogger.