Makonda amponda Kikwete


PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli ni bora kuliko serikali ya awamu ya nne.

Makonda ambaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni katika utawala wa awamu ya nne chini ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, amesema serikali iliyopita ilikuwa na matabaka kati ya viongozi na wananchi tofauti na ilivyo sasa.


Makonda alikuwa akizungumza leo katika kipindi cha Terminal cha Clouds Fm leo alasiri.

“Serikali ya sasa inafanya kazi nzuri zaidi. Kuna tofauti kubwa kati ya ya watawala na viongozi kwa sababu kiongozi anasifa ya kuwasikiliza anaowaongoza lakini mtawala hana sifa hiyo,” amesema Makonda.

Amejinasibu kuwa Mkoa wake wa Dar es Salaam umekuwa Mkoa wa kipekee kwani viongozi wanashirikiana na wananchi moja kwa moja.

No comments:

Powered by Blogger.