Baada ya miaka 10 Materazzi kaweka wazi kilichomfanya apigwe na Zidane
Beki wa kati wa zamani wa timu ya taifa ya
Italia na klabu ya Inter Milan ya Italia Marco Materazzi,
usiku wa July 8 2016
ameamua kuweka wazi kilichomfanya apigwe na nahodha wa
zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa ambaye kwa sasa ni kocha wa Real Madrid Zidane.
Marco Materazzi ameweka wazi
kilichomfanya Zidane ampige kichwa katika mchezo wa fainali
ya Kombe la dunia 2006, tofauti na ilivyokuwa inaripotiwa na wengi, Materraziamekuwa
akiombwa na vyombo mbalimbali vya habari duniani lakini alikuwa akikwepa
kuzungumzia suala hilo
“Toka 2006 nimekuwa nikipokea maombi mengi ya kufanya
interview, nimeamua kutoa kitabu kinachoeleza ukweli kwa sababu kila mtu
anauliza ni nini nilimwambia Zidane hadi akapandwa na hasira na kunipiga
kichwa, ni kweli maneno yangu yalikuwa ya kijinga lakini Zidane hakustahili
kureact vile”
No comments: