Madhara ya Spika na/Au Naibu Kuwa Mteule wa Rais sasa Yanaonekana



Sio siri tena kuwa Dr. Tulia aliteuliwa na Dr. Magufuli awe Mbunge kwa lengo la kupata
nafasi ya Unaibu Spika baada ya mpango wake wa kugombea Uspika kuonekana kugonga mwamba.

Aliyemshinikiza Rais Magufuli kuwa Dr. Tulia ana weledi wa kuweza kuwa Naibu Spika hatumjui lakini ni wazi alimdanganya au Tulia mwenyewe ndiye amejisahau na kudhani kwa vile cheo hicho kapigiwa chapuo na Rais basi Spika sio chochote wala wabunge hawana cha kumfanya.

Ni wazi analivuruga bunge na litavurugika hasa. Haelewani na uongozi wa Bunge kwa kukurupuka kwake, na ana haribu mahusiano ya serikali na wabunge wa pande zote kwa kudhani anaiokoa serikali ya mteule wake.

Amesaidia kuweka wazi kuwa mteule wa Rais hapaswi kuongoza muhimili unaoisimamia serikali. Njia sahihi kabla mambo hayajaharibika kabisa ni yeye kujiuzulu

No comments:

Powered by Blogger.