Wanawake wa Kichagga na Kihaya Mtatumaliza Wanaume


Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Wanawake wa kichagga na kihaya wanatumalizia ndugu zetu. Yaani hawa wanawake ni so strategic, wananyatia wanaume (hata simba na ufundi wake wa kuwinda hawafikii) wenye mafanikio au dalili ya kufanikiwa tu! Wanaume waliosoma, wenye hela au biashara kubwa kubwa. Mbaya zaidi wakishaolewa wanawaendesha hao wanaume mpaka wengine wanakufa vifo vya ghafla kama vile kwa presha! Mrengo wao kimaisha ni kujenga kwao.

Ndugu zangu na rafiki zangu asilimia kubwa wenye mafanikio na elimu wote wameoa wachagga au wahaya, yaani badala ya kuwapenda hawa wanawake kwa sababu ni shemeji zangu, badala yake sina amsha amsha nao kabisa. Mwaka jana kulikuwa na harusi kama 18 hivi ambazo nilihusishwa kwa sababu ya ukaribu au undugu, yaani kati ya hizo 16 mchagga au mhaya anaolewa! Niligoma mgomo baridi, vikao wala michango sikutoa! Mbaya zaidi kuna jamaa nimesom naye UDSM rafiki wa damu, tuliapa viapo vyote, tukae mbali na wanawake wa kichagga na kihaya, cha ajabu juzi ananitumia ujumbe wa simu kuwa anaoa na nilivyohoji shemeji ni wa wapi, akaniambia mchagga. Yaani anamezwa na zimu tulilolikwepa kwa zaidi ya miaka kumi!

Wakuu hii hali ikoje kwa jamaa/ndugu zenu? Wanawake wa kihaya na kichagga muwe na uungwana japo kidogo.

By Simplicity.

No comments:

Powered by Blogger.