DIAMOND AFANYA TUKIO LA KUTISHA INCHINI KENYA, WATU WABAKI MIDOMO WAZI NA KUSHANGAA


Video za muziki wa Bongo Flava kutoka Tanzania ndizo zilizotazamwa zaidi na Wakenya katika mtandao wa YouTube, unaomilikiwa na Google, mwaka huu, takwimu zinaonyesha.
Video hizo zinatawala katika orodha ya video kumi zilizotazamwa zaidi, inayoongoza ikiwa video ya wimbo Salome, uliofanywa upya na Diamond Platnumz na Rayvanny.
Wimbo wa Work, wao Rihanna na Drake ni wa pili lakini kutoka hapo anaingia Diamond Platnumz na Harmonize wakiwa na wimbo wao Bado.
Video ya kwanza ya Wakenya kwenye orodha hiyo ni ya Sauti Sol kwa wimbo wao Unconditionally Bae, lakini bado kwenye wimbo huo walishirikiana na mwanamuziki Mtanzania, Alikiba.
Video nyingine za nyimbo katika orodha hiyo ni Work from Home wa Mmarekani Ty Dolla Sign na kundi la wasichana la Fifth Harmony, This is What You Came For wake raia wa Scotland Calvin Harris, Kwetu wake Rayvanny kutoka Tanzania, Cheap Thrills wao raia wa Australia Sia na Sean Paul wa Jamaica, Pillow Talk wa Mwingereza Zayn na Ain't Your Mama wa Mmarekani Jenniffer Lopez.

BBC SWAHILI

No comments:

Powered by Blogger.