Mashabiki wa Yanga wayachoma moto magazeti yanayo milikiwa na Reginald Mengi.

Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The
Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MEDIA ambayo ipo chini ya Reginald Mengi.

Wanachama na mashabiki wamefikia hatua hiyo baada ya kukasirishwa na kitendo cha Reginald Mengi kutumia vyombo vyake vya habari kuandika habari za uongo na uchochezi kuhusu Yusuph Manji ili kuivuruga Yanga. Mengi ambaye pia ni mwanachama wa Yanga anaonyesha kutofurahishwa kwake na uwepo wa Manji katika klabu ya Yanga.

No comments:

Powered by Blogger.