Wabunge CCM Kumpigia Makofi Kitwanga Kipindi Anajibu Swali Ina Maana Gani

Aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga kabla hajafukuzwa uwaziri alikua
akipigiwa makofi na wabunge wa CCM ndani ya bunge wakati akijibu swali aliloulizwa huku akiwa amelewa,

Najiuliza maswali mengi sana kuhusu waziri Huyu kupigiwa makofi wakati inaonekana hakuwa anajibu swali kiufasaha,

Je wabunge wa CCM walijua ni kwanini walikua wanapiga makofi?
Je wabunge wa ccm walikua makini kweli kujua Kitwanga alichokua akijibu?
Je hawa wabunge walilielewa swali aliloulizwa Kitwanga kabla hawajapiga makofi juu yake?
Kama wabunge walimpigia makofi baadae ilionekana usahili wa alichojibu hakikuoneka kulingana na swali lenyewe na IKULU iko Dar lakini ikamuona hayuko sawa kuanzia kimwili mpaka kiakili, inakuaje wabunge wako karibu na Kitwanga kwenye viti wakashindwa Pata utimamu wa akili na kumpigia mlevi huku haoneshi uhalisia wa kimwili na majibu ya swali husika???

No comments:

Powered by Blogger.