Diamond, Wizkid, Flavour kutumbuiza Barclays Center, New York, July 22

Ni ukumbi wa ndani kwa ndani maarufu mno jijini New York, Marekani nyumbani kwa wasanii wakubwa
wakiwemo Jay Z, Beyonce, Justin Bieber, Rihanna, Drake, taja kila msanii mkubwa wa Marekani, amewahi kutumbuiza hapo.
13098991_975366752531761_1568595609_n
Na sasa Diamond, Wizkid na Flavour, watakuwa wasanii wa kwanza wanaofanyia muziki Afrika kuwahi kutumbuiza kwenye ukumbi huo. Mastaa hao watatumbuiza kwenye tamasha la muziki la One Africa July 22, 2016 kwenye ukumbi huo wenye uwezo wa kujaza watu 20,000.
06BIEBER1-master768

Justin Bieber akitumbuiza kwenye ukumbi wa Barclays Center
“We are about to Make a History America!!!…. Platnumz Diamond with my Fellow African brothers and Sisters will be Shutting the Barclays Center Down! On the 22nd Jully 2016 in New York!…. 20k Seat Capacity!…Now make sure you tell your Friend to tell a Friend,” ameandika Diamond.
beyonce-and-jay-z-barclays-center

Beyonce na Jay Z wakitumbuiza kwenye ukumbi huo
Barclays Center ni ukumbi unaotumika kwa shughuli mbalimbali na upo Brooklyn, New York City. Pia hutumika kama uwanja wa nyumbani wa timu ya kikapu ya Brooklyn Nets pamoja na New York Islanders ya National Hockey League.
20130506-rihanna-2-600x-1367852187

Rihanna ndani ya Barclays Center
Show ya kwanza kufanyika kwenye ukumbi huo ilikuwa ya Jay Z, September 28, 2012.
Crowds arrive outside Barclays Center before Brooklyn Nets  played Toronto Raptors in NBA game in New York

No comments:

Powered by Blogger.